publicidade

67 Zakariya, baba yake mtoto, akajazwa Roho Mtakatifu, akatamka ujumbe wa Mungu:

68 "Asifiwe Bwana Mungu wa Israeli, kwani amekuja kuwasaidia na kuwakomboa watu wake.

69 Ametupatia Mwokozi shujaa, mzawa wa Daudi mtumishi wake.

70 Aliahidi hapo kale kwa njia ya manabii wake watakatifu,

71 kwamba atatuokoa mikononi mwa adui zetu na kutoka mikononi mwa wote wanaotuchukia.

72 Alisema atawahurumia wazee wetu, na kukumbuka agano lake takatifu.

73 Kiapo alichomwapia Abrahamu baba yetu, ni kwamba atatujalia sisi

74 tukombolewe kutoka adui zetu, tupate kumtumikia bila hofu,

75 kwa unyofu na uadilifu mbele yake, siku zote za maisha yetu.

76 Nawe mwanangu, utaitwa, nabii wa Mungu Mkuu, utamtangulia Bwana kumtayarishia njia yake;

77 kuwatangazia watu kwamba wataokolewa kwa kuondolewa dhambi zao.

78 Mungu wetu ni mpole na mwenye huruma. Atasababisha pambazuko angavu la ukombozi litujie kutoka juu,

79 na kuwaangazia wote wanaokaa katika giza kuu la kifo, aongoze hatua zetu katika njia ya amani."