4 Yosefu pia alifanya safari kutoka mjini Nazareti mkoani Galilaya. Kwa kuwa alikuwa wa jamaa na ukoo wa Daudi alikwenda mjini Bethlehemu mkoani Yuda alikozaliwa Mfalme Daudi.5 Alikwenda kujiandikisha pamoja na mchumba wake Maria ambaye alikuwa mja mzito.6 Walipokuwa huko, siku yake ya kujifungua ikawadia,7 akajifungua mtoto wake wa kwanza wa kiume, akamvika nguo za kitoto, akamlaza horini kwa sababu hawakupata nafasi katika nyumba ya wageni.
publicidade